Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele ametangaza marekebisho ya orodha ya maeneo ya uchaguzi kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025
Imewekwa: 12 Oct, 2025

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele amezungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo Oktoba 12, 2025 na kutangaza marekebisho ya orodha ya maeneo ya uchaguzi kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .
Mhe.Jaji Mwambegele amesema marekebisho hayo yamefanyika kufuatia kufutwa kwa baadhi ya maeneo na ametangaza kutengua uteuzi wa wagombea saba katika maeneo ya uchaguzi yaliyofutwa, kufutwa kwa vituo vya kupigia kura 292 katika kata zilizofutwa na kuanzishwa kwa vituo vingine 292 katika Kata walipohamishiwa wapiga kura husika.